Kabla hujaanzisha jumuiya yako, bainisha unalokusudia – je, ni kusimamia miradi mashinani, kutoa usaidizi wa kijamii moja kwa moja kwa wanaohitaji, kuhamasisha kuhusu suala fulani, au kitu kingine? Lengo lako litakusaidia kubainisha wahusika utakaowajumuisha kwenye jumuiya na ni vikundi gani wataingia. Unaweza kuanzisha au kuongeza vikundi vya:
- wanaojitolea kulingana na eneo la kijiografia;
- wanaojitolea kulingana na ujuzi wao;
- wanaojitolea kulingana na mradi au tukio;
- wasimamizi wa mradi au waratibu wa wanaojitolea;
- wahusika wapya wa kujitolea wanaohitaji mafunzo;
- wahusika wanaojitolea wa kukusanya na kushiriki mbinu bora;
- wanaojitolea waliopewa jukumu la kukusanya na kushiriki simulizi kuhusu mabadiliko ya mpango;
- Wanaonufaika na misaada kulingana na mahitaji au kuathirika kwao;
- Wanaonufaika na misaada kulingana na eneo la kijiografia;
- wafadhili kulingana na mradi au kinachowavutia.
Kuwa na lengo bayana la jumuiya kutawasaidia wasimamizi wako na wanajumuiya kuelewa sababu za kuongezwa au kutoongezwa kwenye vikundi fulani. Kwa mfano, ikiwa sehemu ya lengo lako ni kutoa chakula kwa familia zenye mapato ya chini, unaweza kuanzisha au kuongeza kikundi cha utayarishaji na usafirishaji wa chakula, na pia kikundi cha waliojitolea ambao jukumu lao ni kutoa mafunzo kwa wanajumuiya wapya. Kwa upande mwingine, kikundi cha wanaojitolea ambao wanaungana kwa lengo la kupiga soga kuhusu jambo linalowavutia hakitaongezwa.