Salama ilivyokusudiwa
Ili kukuweka salama, tumeunda hali ya utumaji ujumbe na kupiga simu kwa usalama wa hali ya juu, tumeunda zana bunifu ili kukuweka kuwa na udhibiti, na tuko tayari kukusaidia unapohitaji.
Ili kukuweka salama, tumeunda hali ya utumaji ujumbe na kupiga simu kwa usalama wa hali ya juu, tumeunda zana bunifu ili kukuweka kuwa na udhibiti, na tuko tayari kukusaidia unapohitaji.
Hakuna mtu anayeweza kutafuta nambari yako ya simu au kusoma ujumbe wako wa kibinafsi.
Tunakamata na kuondoa akaunti nyingi za barua taka na za ulaghai kabla hata ziweze kukufikia au kabla ya mtu yeyote kuziripoti.
Tunakuomba kuthibitisha utambulisho wako ikiwa tutagundua majaribio yoyote ya kutiliwa shaka au ambayo hayajaidhinishwa kuchukua akaunti yako.
Angalia hatua hizi rahisi ambazo zitaongeza safu za ziada za ulinzi ili kuzuia wavamizi na walaghai wasiibe akaunti na data yako.
Sanidi pin ya siri na usiwahi kuishiriki na mtu yeyote ili kuzuia mtu kuiba akaunti yako.
Kutumia matoleo ghushi ya WhatsApp huleta hatari kubwa za faragha na usalama kwa akaunti na data yako.
Dhibiti ni nani anayeweza kukuongeza kwenye vikundi na nani anaweza kujiunga na vikundi vyako, na kuwaondoa wanachama au ujumbe inapohitajika.
Jua ulaghai na hatua za kawaida unazoweza kuchukua ili kujilinda wewe na wapendwa wako.
Kuripoti ujumbe, watu au biashara hutusaidia kuweka WhatsApp salama kwa kila mtu. Usijali, hatutamtaja mtumaji.
Ikiwa mtu ambaye hutaki kupiga gumzo naye anakutumia ujumbe, mzuie tu na tutahakikisha kuwa hutapokea tena ujumbe au simu zake.
Ikiwa umepoteza ufikiaji wa akaunti yako, sajili tena nambari yako ya simu. Mazungumzo ya awali ni salama kwenye simu yako na hayawezi kusomwa na mtu yeyote anayejaribu kufikia akaunti yako.
Vikundi vya WhatsApp vinaendelea kukuunganisha na familia, marafiki, wafanyakazi wenzako, wanafunzi wenzako, na zaidi. Vile watu wanavyotumia vikundi kwa mazungumzo muhimu, watumiaji wameomba udhibiti zaidi juu ya hali yao. Leo, tunaanzisha mipangilio ya faragha mpya na mfumo wa kukaribisha ili kukusaidia kuamua ni nani anayeweza kukuongeza kwenye vikundi.
Lengo letu ni kufanikisha mawasiliano duniani kwa faragha. Huku mawasiliano yetu mengi yakizidi kuhamia mifumo ya dijitali kutoka ana kwa ana, tunatambua kwamba kuna upekee fulani wa kuketi na mtu na kushauriana naye uso kwa macho, mkielezana mawazo yenu kwa ujasiri, mkifahamu kwamba mnawasiliana kwa faragha na kwa wakati halisi. Uhuru wa kusema ukweli na kufungua roho, huku mkijua kwamba mazungumzo yenu hayanakiliwi na kuhifadhiwa mahali fulani milele.
Tunaamini kuwa ujumbe unapaswa kuwa wa faragha na salama. Usimbaji fiche kutoka mwisho hadi mwisho ndio msingi, na tutaunda vipengele vipya kila wakati ili kutoa tabaka za ziada za faragha.