Hatuwezi kuona maudhui ya ujumbe wa kibinafsi kwa sababu umefumbwa mwisho hadi mwisho. Isitoshe, hatuweki kumbukumbu za ni nani kila mtu anatumia ujumbe au kupigia simu. Tunadhani kuweka rekodi za kibinafsi za watumiaji bilioni tatu kutakuwa mbaya kwa faragha na huwa hatuziweki.
Tuna uwezo wa kuelewa jinsi ambavyo vipengele vyetu vinatumiwa ili tuendelee kuviboresha, na tunalenga kuondoa maelezo ya kibinafsi tunapofanya hivi. Tumeunda teknolojia inayoondoa maelezo ya kibinafsi ambayo yanaweza kuhusishwa na mtu au nambari mahususi ya simu kama ilivyoelezwa hapa.
Pia tunashughulika ili kugundua barua taka au matumizi mabaya kupitia mifumo na ripoti za kiotomatiki za kina. Kwa mfano, mtumiaji anayetuma ujumbe 1,000 kwa dakika moja huenda ni akaunti ya barua taka ya kiotomatiki na tutataka kuwapiga marufuku kutumia WhatsApp. Katika visa vya matumizi mabaya kama hii, tuna uwezo wa kuona ni nani anamtumia nani ujumbe pindi tu baada ya tatizo kutambuliwa.
Kwa sababu tuna uwezo huu, wakati mwingine huwa tunapokea maagizo ya kisheria ili kutoa maelezo haya. Tuko wazi kuhusu jinsi tunavyojibu maombi halali ya utekelezaji wa sheria na unaweza kupata maelezo zaidi hapa.